SAFARI ZA TRENI KATI YA KILOSA NA GULWE ZAREJEA TENA RASMI - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Monday, February 12, 2018

SAFARI ZA TRENI KATI YA KILOSA NA GULWE ZAREJEA TENA RASMI


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame M. Mbarawa amezindua rasmi safari za treni katika eneo la Kilosa na Gulwe ambalo lilikuwa limeathirika kutokana na mvua zilizosababisha uharibifu wa miunbombinu ya reli katika eneo hilo na kusimama kwa safari kwa takribani mwezi mmoja. Waziri Mbarawa katika ziara hiyo aliyoifanya jana Tareh 11 February, ambapo alifungua njia hiyo kwa kuendesha treni ya mizigo yenye behewa 20 kama ishara ya kurudisha upya safari za treni kutoka Dar es Salaam kuelekea Bara.
Aidha katika ziara hiyo Waziri Mbarawa ameeleza kuwa kutokana na kusimama kwa safari za treni za mizigo na abiria kwa kipindi cha mwezi mmoja TRL imepoteza takriban Bilioni 4 na amewahakikishia watumiaji wa usafiri huo kuwa huduma zimerejea.
Mkurugenzi wa TRL Ndg. Masanja Kadogosa akipeperusha bendera kuruhusu treni iliyokuwa ikiendeshwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kuashiria ufunguzi wa safari za treni kati ya Kilosa na Gulwe.
Mara baada ya kukagua ukarabati wa reli unaofanyika katika eneo hilo, Waziri Prof. Mbarawa aliwatoa hofu wafanyabiashara wanaotumia usafiri wa treni za reli ya kati kuwa mizigo yao iko salama, na kuwa kampuni ya reli imejipanga kutoa huduma bora zaidi, pia Waziri Mbarawa aliongeza kwa kusema kuwa kuanzia sasa hivi mvua zinazokuja mwezi wa tatu na wa nne reli itakuwa salama, waendelee kutumia huduma za usafiri wa treni.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akipanda kwenye injini ya treni kwa ajili ya kuendesha kuashiria kuanza rasmi kwa safari treni kati ya Kilosa na Gulwe
“Tuna kampuni ya reli ya kisasa na tumejipanga zaidi kutoa huduma kwao wao iliyotukuka, mizigo yao iko salama”, “Changamoto zilizotokea zimetokea ila nataka kuwahakikishia kwamba kuanzia sasa hivi mvua zinazokuja mwezi wa tatu na mwezi wa nne reli itakuwa salama na waendelee kuiamini reli yetu” Alisema Mbarawa.
Pia Waziri Mbarawa alitoa wito kwa vibarua wanaofanya kazi kwenye ukarabati wa njia hiyo ya reli na kuwataka wawe waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku wawapo kazini ili kuepuka udokozi unaoweza kuisababishia hasara serikali.

Mkurugenzi wa TRL akizungumza na wananchi wa maeneo ya Kilosa mara baada ya ufunguzi wa safari za treni kati ya Kilosa na Gulwe


Mkurugenzi wa TRL Ndg. Masanja Kadogosa akishiriki kazi na baadhi ya vibarua wanaoshiriki kwenyenukarabati wa reli kati ya Kilosa na Gulwe.

No comments:

Post a Comment