UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA KOROGWE NA MOMBO UMEKAMILIKA KWA 90% - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Wednesday, November 29, 2017

UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA KOROGWE NA MOMBO UMEKAMILIKA KWA 90%


Kazi ya ukarabati wa njia ya reli kati ya Tanga na Arusha inaendelea. Mafundi wa Kampuni ya Reli Tanzania bado wapo kazini, ambapo ukarabati wa awamu ya awali kati ya Korogwe na Mombo upo mbioni kukamilika, bado Km 5 tu hadi kufika Stesheni ya Mombo.

Ukarabati huo wa njia ya reli ya Tanga na Arusha yenye urefu wa Km 437 unaotarajiwa kukamilika mwaka 2018 mwezi Juni, unahusisha uwekaji mataluma na reli katika maeneo yaliyoathirika kutokana na wizi wa miundombinu ya reli unaofanywa na baadhi ya wananchi wasio waaminifu, pamoja na usafi wa njia hiyo ikiwemo uondoaji wa nyasi na miti iliyoota kwenye njia hiyo.

Matukio zaidi katika picha





Ukarabati wa wa njia ya reli ya Tanga na Arusha umelenga kurudisha upya safari za treni kwa abiria na mizigo ambazo zilikuwa zimesimama kwa muda mrefu, ufufuaji huo utahusisha pia matengenezo makubwa na madogo ya Vituo vya treni na magenge ya wafanyakazi yaliyopo katika njia hiyo ya reli.



Sehemu ya ofisi ya kituo cha treni cha Korogwe ikiwa tayari imefanyiwa ukarabati mdogo katika baadhi ya sehemu ukijumuisha fenicha na majengo ya ofisi ya kituo hicho.

              

1 comment:

  1. NAPONGEZA HATUA YA KUIFUFUA RELI HIYO YA TANGA ARUSHA, NAKUMBUKA MIAKA YA NYUMA NILITUMIA USAFIRI SANA WA TRENI HIYO KWENDA MOSHI, NA KUNA DEREVA WA GARI MOSHI WA NJIA HIYO ALIKUWA MAARUFU JINA LAKE ALIKUWA AKIITWA YONA, ILA NASIKIA KWA SASA NI MAREHEMU>

    ReplyDelete