PICHA; UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA TANGA NA ARUSHA UNAENDELEA KWA KASI - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Friday, November 10, 2017

PICHA; UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA TANGA NA ARUSHA UNAENDELEA KWA KASI


Ukarabati wa njia ya reli kati ya Tanga na Arusha unaendelea kwa kasi, ambapo kwa hivi sasa mafundi wanakarabati kipande cha reli kati ya Korogwe na Mombo. Tayari Km 27 kati ya Km 46 za kipande hicho cha njia ya reli umekamilika, huku mafundi wakiendelea na km 19 zilizobaki hadi kufika stesheni ya Mombo.
Ukarabati wa njia hiyo ya reli ambao ulianza tarehe 02 Oktoba 2017 unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka 2017 kwa kipande cha Korogwe hadi Mombo.
Kukamilika kwa ukarabati huo kunatarajiwa kusaidia shughuli nyingi za kiuchumi, kijamii pamoja kuongeza ajira kupitia usafiri wa reli ambao ulikuwa umezorota katika njia hiyo tangu mwaka 2008 na kuathiri shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii.


Mafundi wakipakia mataluma na vyuma vya reli katika Stesheni ya Korogwe kwa ajili ya kwenda kufanyia ukarabati sehemu za njia ya reli zilizoharibika kutokana na wizi wa vyuma vya reli.

Mafundi wakiwa wamebeba vyuma vya reli kuvipeleka katika sehemu inayotakiwa kufanyiwa ukarabati.

Mafundi wakiondoa kifusi kilichofunika njia ya reli katika eneo la Makuyuni
Mafundi wakiendelea na kazi ya kusafisha njia ya Reli katika eneo la Makuyuni

Mafundi wakifunga vyuma vya reli kwenye mataluma katika makutano ya njia ya reli na barabara eneo la Makuyuni
Mafundi wakifunga vyuma vya reli kwenye mataluma katika makutano ya njia ya reli na barabara eneo la Makuyuni

Mafundi wakifunga vyuma vya reli kwenye mataluma katika makutano ya njia ya reli na barabara eneo la Makuyuni





Sehemu ya njia ya reli katika eneo la Makuyuni ikiwa tayari imefanyiwa usafi na kuondolewa kifusi kilichofunika reli


No comments:

Post a Comment