MKURUGENZI WA TRL NA RAHCO AFANYA MKUTANO NA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI HIZO MBILI - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Thursday, November 2, 2017

MKURUGENZI WA TRL NA RAHCO AFANYA MKUTANO NA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI HIZO MBILI

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Ndg. Masanja Kungu Kadogosa amefanya mkutano na wafanyakazi wa TRL na RAHCO ili kujadili utendaji kazi wa kampuni hizo mbili na namna ya kuendelea kuboresha utendaji kazi wa kampuni hizo mbili kwa lengo la kuongeza ufanisi katika usafiri wa reli Tanzania.
Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania Ndg. Masanja Kungu Kadogosa akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania na Kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli.
Kadogosa alizungumzia kuhusu mabadiliko ambayo yanatarajiwa kutokea kwenye kampuni hizo mbili, ambapo linatarajiwa kuundwa shirika moja ambalo litakuwa linashughulika na shuhguli zote za reli ikiwemo ujenzi, usimamiaji wa rasilimali za reli na utoaji wa huduma za reli,na kuwataka wafanyakazi kuwa tayari na mabadiliko hayo ili kwenda sambamba na kasi ya serikali katika ufanyaji kazi.
Pia Mkurugenzi Kadogosa alisema kuwa mabadiliko yanayotarajiwa kutokea yatakuwa ni makubwa yatahusisha mabadiliko ya fenicha za maofisini, magari pamoja na hali bora ya kiutendaji
“TRC tunayokwenda sio ile iliokuwa hata ‘organization’ sio ile tuliyokuwa nayo ila itakuwa ni ya tofauti”, “Kuna watu hawapendi haya mabadiliko, mabadiliko yanayokuja ni makubwa ikiwemo magari sehemu zote, Dar es salaam, Morogoro, Tabora, fenicha za maofisini pia na hali bora ya kiutendaji” alisema Ndg. Kadogosa
Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania Ndg. Masanja Kungu Kadogosa akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya Reli Tanzania na Kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli
Pamoja na hayo Ndg. Kadogosa amesisitiza kuwa serikali haina mpango wa kumuachisha mtu kazi isipokuwa kwa wale watakaojitakia wenyewe, pia amesisistiza kuwa serikali kupitia wizara itaunda kamati itakayosimamia suala zima la kuundwa kwa Shirika jipya la Reli litakalotokana na RAHCO na TRL ambapo litaitwa Tanzania Railyways Cooperation (TRC). Na itawekwa wazi ni kwa namna gani kampuni hizo mbili zitaungana na namna ambavyo maslahi ya wafanyakazi yakavyowekwa, pia amesisitiza kuwa hakuna mfanyakazi atakayepunguziwa mshahara. 
Mkurugenzi mkuu wa Uendeshaji wa Kampuni ya Reli Tanzania Ndg. Masanja Kungu Kadogosa akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania na Kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli
Wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu Ndg. Masanja Kungu Kadogosa
Mmoja wa wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania akiuliza swali kwa Menejimenti.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu Ndg. Masanja Kungu Kadogosa


No comments:

Post a Comment