KAMPUNI YA RELI KURUDISHA SAFARI ZA TRENI KATI YA DAR ES SALAAM, TANGA NA ARUSHA - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Monday, October 30, 2017

KAMPUNI YA RELI KURUDISHA SAFARI ZA TRENI KATI YA DAR ES SALAAM, TANGA NA ARUSHA

Kampuni ya Reli Tanzania imeanza kazi ya kurudisha huduma ya usafiri wa mizigo na abiria kati ya Tanga na Arusha ambayo ilisitishwa kwa takribani muda wa miaka kumi tangu mwaka 2008 kutokana na changamoto za kiutendaji, hatua hiyo ni moja kati ya mikakati ya kampuni katika kuboresha huduma ya usafiri wa abiria na usafirishaji mizigo nchini Tanzania.
Kipande cha reli kati ya Stesheni ya Korogwe na Maurui kikiwa tayari kimefanyiwa ukarabati.
Maboresho ambayo yapo mbioni kumalizika na kuanza safari zake mara tu matengenezo ya reli yatakapokamilika ni kutoka Dar es salaam hadi Mombo na kuanza safari zake mara moja baada ya kukamilika.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi za Kampuni ya Reli Tanzania Mkurugenzi Mkuu Ndg. Masanja Kungu Kadogosa amesema kuwa ufufuaji wa njia hiyo ya reli utaleta ufanisi kwenye kurahisisha shughuli za kiuchumi katika Mikoa ya Tanga na Arusha.
Ndg. Masanja ameongeza kuwa ukarabati huo unakwenda kwa kasi hadi kufikia mapema mwakani safari za treni za mizigo na abiria kati ya Dar es Salaa na Tanga kwenye stesheni ya Mombo utakuwa umeanza kufanya kazi ikiwa ni awamu ya kwanza huku mafundi wakiendelea na ukarabati wa njia hiyo ili kutimiza lengo la kurudisha safari za treni hadi Arusha. 
Mafundi wakiweka kifusi katika tuta la reli ambalo lilikuwa limeathirika na mmomonyoko wa udongo.
Picha zaidi; Mafundi wakiendelea na uondoaji kifusi kilichofunika njia ya reli ya Tanga-Arusha pamoja na uondoaji wa nyasi na miti iliyoota kwenye njia hiyo.  









No comments:

Post a Comment