NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI ATEMBELEA OFISI ZA KAMPUNI YA RELI NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MENEJIMENTI - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Monday, October 30, 2017

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI ATEMBELEA OFISI ZA KAMPUNI YA RELI NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MENEJIMENTI

Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye ambaye ni naibu waziri mpya wa Uchukuzi na Mawasiliano baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mabadiliko madogo ya wizara, mawaziri na manaibu mawaziri.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Anditiye akizungumza na Menejimenti ya TRL pamoja na waandishi wa habari wasili katika ofisi za TRL jijini Dar es Salaam
Naibu waziri Anditiye amefanya ziara hiyo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake katika taasisi za uchukuzi na mawasiliano nchini, kwa lengo la kupata taarifa za maendeleo ya miradi mbalimbali ya taasisi zilizo chini ya wizara ya uchukuzi na mawasiliano ikiwemo Kampuni ya Reli Tanzania.
Katika ziara hiyo Naibu waziri Mhandisi Anditiye amepatiwa taarifa za miradi mbali mbali ya Kampuni ya Reli Tanzania ikiwemo mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa inayotumia umeme(SGR) ambao mpaka hivi sasa umetimu miezi sita, mradi wa ufufuaji wa reli kati ya Tanga na Arusha, treni za abiria za mjini na zinazoenda mikoani pamoja na zile zinazoenda mjini.

Mkurugenzi Mkuu Ndg. Masanja Kungu Kadogosa akizungumza na waandishi wa habari waliofika kwenye ziara ya Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliani Mhandisi Atashasta Anditiye katika ofisi za TRL jijini Dar.
Pia Mhandisi Anditiye amepatiwa taarifa za hatua za ziada ambazo Kampuni ya reli zinachukua kuboresha huduma za usafiri wa reli nchini. Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji Ndg. Focus Sahani amemueleza naibu waziri kuwa kampuni imefanyia ukarabati wa njia za reli, mabehewa na injini.
Aidha Mkurugenzi Mkuu Ndg. Masanja Kungu Kadogosa ameeleza mafanikio ambayo mpaka sasa kampuni ya Reli Tanzania limepata kufuatia uboreshaji wa huduma ya usafiri wa reli Tanzania. 
Naye naibu Waziri Atashasta Anditiye ameahidi ushirikiano kwa Kampuni ya Reli Tanzania katika kuhakikisha utendaji kazi unaimarika zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji Ndg. Focus Sahani akitoa taarifa ya shughuli ambazo TRL inafanya na mipango iliyopo kwa ajili ya kuboresha huduma kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliani Mhandisi Atashasta Anditiye katika ofisi za TRL jijini Dar.
Mkurugenzi Mkuu wa TRL Ndg. Masanja Kungu Kadogosa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Anditiye mara baada ya kuwasili katika ofisi za TRL jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment