MKURUGENZI MKUU WA UENDESHAJI WA TRL NDG. FOCUS SAHANI ATEMBELEA UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA TANGA NA ARUSHA - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Monday, October 30, 2017

MKURUGENZI MKUU WA UENDESHAJI WA TRL NDG. FOCUS SAHANI ATEMBELEA UKARABATI WA NJIA YA RELI KATI YA TANGA NA ARUSHA

Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji wa Kampuni ya Reli Tanzania Ndg. Focus Sahani ametembelea ukarabati wa njia ya reli kati ya Tanga na Arusha katika eneo la stesheni ya Maurui, iliyopo Wilayani Korogwe mkaoni Tanga.

Ndg. Sahani ameridhishwa na utendaji kazi wa mafundi ambao wanafanya ukarabati wa njia hiyo tangu mwezi Agosti na mpaka sasa zaidi ya KM 16 zimekamilika, huku km 30 zikibaki kufanyiwa ukarabati hadi kufika Stesheni ya Mombo. Ukarabati huu ni wa awamu ya kwanza ambao unaanzia Stesheni ya Korogwe hadi Mombo.
Ukarabati wa njia hiyo unahusisha usafishaji wa njia hiyo ikiwemo kuondoa vifusi vilivyokuwa vimefunika reli, kuondoa nyasi, miti pamoja na visiki vilivyokuwa vimeota kwenye njia hiyo kutokana na kutotumika kwa njia hiyo ya reli kwa muda mrefu.

Lengo la ukarabati wa njia hiyo ya reli ni kurudisha safari za abiria na mizigo kutoka Stesheni ya Dar es salaam hadi Tanga, Moshi na Arusha ambayo itasaidia katika kukuza uchumi lakini pia kuboresha huduma ya usafiri wa reli nchini. 
Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji Ndg. Focus Sahani akisalimiana na Mhandisi Vitalis Magohagasenga mara baada ya kufika stesheni ya Maurui kutizama matengenezo ya njia ya reli kati ya Tanga na Arusha
Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji Ndg. Focus Sahani akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRL wanaofanya kazi ya kukarabati njia ya reli eneo la stesheni ya Maurui.
Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji Ndg. Focus Sahani akipata ufafanuzi kutoka kwa Mhanidisi Vitalis Magohagasenga kuhusu kukarabati njia ya reli eneo la stesheni ya Maurui

No comments:

Post a Comment