MAFUNDI WA TRL WAENDELEA NA KAZI YA KUFANYIA UKARABATI KICHWA CHA TRENI KILICHOKUWA KIKITUMIA MAKAA YA MAWE - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Monday, October 30, 2017

MAFUNDI WA TRL WAENDELEA NA KAZI YA KUFANYIA UKARABATI KICHWA CHA TRENI KILICHOKUWA KIKITUMIA MAKAA YA MAWE

Kampuni ya Reli Tanzania katika kuhakikisha linatoa huduma inayoendana sambamba na kasi ya serikali ya awamu ya tano, imeamua kufufua kichwa cha treni aina ya SUK 2927 ambacho kilikuwa kinatumia makaa ya mawe kama nishati ya kuendeshea chombo hiko.
Kichwa hiko kilichokuwa miongoni mwa vichwa arobaini vya aina hiyo vilivyokuwa vikifanya shughuli ya usafirishaji wa mizigo na abiria nchini Tanzania na Afirca Mashariki kuanzia mwaka 1954, kinafanyiwa matengenezo ili kirudi kati shughuli hiyo ya usafirishaji mizigo na abiria ili kuongeza kasi ya ufanisi ya utoaji huduma, lakini pia kichwa hiko cha treni kinaweza kuwa sehemu ya Utalii kutokana na Historia iliyoibeba.

Kichwa hiko kwa hivi sasa hakitumii tena nishati ya makaa ya mawe, bali kinatumia nishati ya mafuta ya dizeli ambapo mfumo wa matumizi ya makaa ya mawe ulibadilishwa mwaka  1998 na kuanza kutumia nishati ya mafuta ya dizeli. 








No comments:

Post a Comment