TANZANIA NA RWANDA KUJENGA RELI YA KISASA KUTOKA ISAKA HADI KIGALI - TRC Blog

Home Top Ad

"TOGETHER WE MOVE"

Thursday, January 18, 2018

TANZANIA NA RWANDA KUJENGA RELI YA KISASA KUTOKA ISAKA HADI KIGALI

Tanzania na Rwanda zimekubaliana kujenga reli ya kisasa(SGR) yenye urefu wa km400 kutoka Isaka-kigali, mradi ambao utasaidia usafirishaji wa bidhaa na kukuza biashara baina ya nchi hizo mbili.
Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya mazungumzo kati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam kufuatia ziara ya kikazi ya siku moja ya Rais Paul Kagame.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais wa Rwanda Paul Kagame
Rais Magufuli amesema kuwa wamewaelekeza mawaziri wa miundombinu wa nchi hizo mbili kukutana wiki inayofuata kujadili namna ya kuwezesha mradi huo kifedha. Mazungumzo hayo ya mawaziri hao wawili yatazingatia namna ya ufadhili wa mradi huo kabla ya kutangazwa tenda, Magufuli amesema kuwa jiwe la msingi litawekwa mwisho mwa mwaka huu 2018.
Reli hiyo inatarajiwa kuunganisha Dar es Salaam na Kigali kupitia Isaka na kuboresha usafirishaji wa bidhaa kutoka ndani na nje ya Rwanda, kwa kuzingatia kwamba takribani asilimia 60 ya mizigo inayotoka na kuingia Rwanda inapitia bandari ya Dar es Salaam.
Mtandao wa reli ya kisasa(SGR) unatarajiwa kuunganisha nchi za Afrika Mashariki, Tanzania, Rwanda, Burundi, Kenya na Uganda ambapo tayari Kenya imejenga reli hiyo ya Kisasa inayounganisha jiji la Mombasa na Nairobi, huku Tanzania na Uganda zikiwa tayari ziemeanza mchakato wa ujenzi wa reli hiyo ya kisasa.
Tanzania inajenga reli ya kisasa (SGR) kwa awamu mbili kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro ambayo itakuwa na urefu wa km330 na Morogoro hadi Makutupora (Dodoma) ambayo itakuwa na urefu km426 zikitumia fedha za ndani takribani dola za kimarekani Bilioni 3.



2 comments:

  1. Ni jambo jema kuona viongozi wetu wana mtazamo wa mbele wa secta hii ua usafirishaji hasa kuhusiana na suala zima la kupunguza gharama na pia kuweza kusafirisha mizingo mingi na mizito ambayo ingepita katika barabara zetu ingesababisha uharibifu wa barabara hizo.
    Na pongeza uamuzi huo walioufikia!

    ReplyDelete
  2. Uncle Magufuli Songa mbele usiangalie wala kugeuka myuma.....wala usisimame wewe kazamwendo tuu.....mpaka kieleweke , big up sana kwako Rais wetu kipenzi.....

    ReplyDelete